Pete ni kifaa cha kuingizwa kidogo kinachojikunga na kinacho kaa ukeni. Unaiwacha ndani kwa wiki 3 kwa wakati na kuitoa wiki ya 4. Pete inazuia mimba kwa njia mbili. Inawachilia homoni ambazo zinazuia ovari kuwachilia yai, na inafanya ute wa shingo ya kizazi uwe nzito na kuzuia mbegu za kiume kufikia yai.
Pete
Ufupisho
Mambo ya haraka
- Rahisi kuingiza
- Inakukinga dhidi ya mimba kwa mwezi 1 kwa wakati.
- Ufanisi: Kwa matumizi kamilifu, wanawake 99 kati ya 100 wataweza kuzuia mimba. Kwa matumizi ya kawaida, ama jinsi watu wengi huitumia, pete huzuia mimba kwa wanawake 91 kati ya 100 wanaoitumia.
- Madhara: Madhara za kawaida zaidi ni utokwaji damu usiyotabirika, ongezeko la mchozo wa uke, ulaini wa matiti au kichefuchefu. Hizi ni za muda mfupi.
- Jitihada: ya wastani. Ingiza pete. Ngoja wiki 3. Toa pete. Ngoja wiki 1. Rudia.
- Haikingi dhidi ya magonjwa ya zinaa (STI).
Maelezo
[8]
Inahitaji jitihada kidogo kiasi kila mwezi. Ikiwa unaogopa sindano, ama wewe ni mtu anayeweza kuwa na shida ya kukumbuka kumeza tembe kila siku, pete ni njia inaweza kukufaa. Unahitaji tu kukumbuka kufanya kitu mara mbili kwa mwezi.
Unapaswa kuridhika na mwili wako. Ikiwa hauwezi kuweka vidole vyako ndani ya uke wako, pengine pete haikufai. Ni kama kuweka tamponi. Ikiwa unaweza kufanya hivyo, basi unaweza kujifundisha kutumia pete.
Unaweza kosa kupata hedhi yako. Pete inakuruhusu kukosa hedhi kabisa, na hili ni salama kwa asilimia 100.
Uhifadhi na faragha. Ukiwa na pete za ziada unaweza zihifadhi katika halijoto ya kawaida kati ya 68°F hadi 77°F (20°C hadi 25°C) kwa hadi miezi 4. Ikiwa utakuwa nazo kupita miezi 4, basi zihifadhi kwenye baridi. Usizitumie ikiwa tarehe ya mwisho kutumika imepita. Ikiwa unataka kuweka siri ya njia yako ya kuzuia mimba, hili ni la kukutia wasiwasi. Pia, wenzi wengine husema wanaweza kuihisi wakati wa ngono. kama hio inaleta shida, basi unaweza kutoa pete wakati unafanya ngono. Ukiitoa wakati wa kufanya ngono, irudishe ndani ya masaa 3. Pia, toa pete mara moja tu ndani ya masaa 24. Kuitoa mara nyingi ama kuitoa na ukose kuirudisha kwa masaa zaidi ya 3 kunarudisha chini ufanisi wake.
Pete inawachilia dozi ya chini ya homoni. Pete ina dozi ya chini ya homoni kuliko njia za uzuiaji mimba zingine. Kunaweza kuwa na madhara hasi chache.
Wavuta sigara wa miaka zaidi ya 35, muwe waangalifu. Kwa wanawake walio na miaka zaidi ya 35, kuvuta sigara wakati unatumia pete kunaongeza hatari ya madhara fulani. Unashauriwa kuzungumzia swala hili na mtoaji wako wa matibabu.
Ni lini naweza kushika mimba tena? Utaweza kushika mimba punde baada ya kutoa pete. Ukitaka kushika mimba, hio ni nzuri sana! Ukitaka kuepuka mimba, ingiza pete ingine au jikinge na njia tofauti.
Jinsi ya kutumia
Pete ni rahisi kutumia. Unachohitaji kukumbuka ni saa za kuingiza na kutoa pete.
Jinsi ya kuiingiza. Kwanza, nawa mikono kwa sabuni na maji. Wacha yakauke yenyewe kwa upepo. Kuingiza pete, ishikilie kati ya kidole gumba na kidole cha shahada na uingize jinsi unavyo weza kuingiza tamponi. Itasimama kwenye pande ya ukuta wa uke wako. Pahali inaposimama kwenye ukuta wa uke haijalishi, bora haikuumizi. Sio lazima uitoe ukifanya ngono. (Ni sawa ukitaka kuitoa ukifanya ngono. Hakikisha tu kwamba unairudisha ndani ya masaa 3. Na uitoe tu mara moja ndani ya masaa 24) [5]
Jinsi ya kuitoa. Ukishaingiza pete, iwache ndani kwa wiki 3. Itoe mwanzo wa wiki ya 4. Iwache nje kwa wiki 1. Kisha ingiza pete mpya na anza mzunguko tena. (Kutoa pete ingiza kidole ushike upindo wa chini wa pete na uivute nje). Pete ikishatoka nje, huenda ukapata hedhi yako.Usijali ikiwa bado unatokwa na damu ikifika wakati wa kuweka pete mpya.Hili ni la kawaida na hedhi yako itaisha punde [6].
Vidokezi na Mbinu. Kuingiza pete, hakikisha umesimama au umeketi vizuri- kwa mfano simama ukiwa umeweka mguu moja juu, chuchuma au ulale chini. Unaweza pia jaribu njia ya “kupinda”ambayo unapinda pete kuiingiza.
Madhara
Kila mtu ni tofauti. Kile unachopitia pengine hakitafanana na mtu mwingine.
Mambo chanya: Kuna vitu vingi kuhusu pete ambavyo ni vizuri kwa mwili wako na pia maisha yako ya ngono [2].
- Rahisi kutumia- Ni kama kuweka tamponi
- Sio lazima ukatize ngono kuitumia
- Inaweza kukupa hedhi nyepesi inayokuja siku chache
- Inaweza kumaliza chunusi
- Inaweza kupunguza maumivu ya tumbo wakati wa hedhi na dalili za kabla ya hedhi (PMS).
- kinakupa kinga dhidi ya matatizo mengine ya kiafya: Saratani ya ndani ya mji wa mimba na saratari ya ovari; anemia ya upungufu wa madini ya chuma; Uvimbe kwenye ovari na ugonjwa wa uvimbe wa fupanyonga
Mambo hasi: Kila mtu huwa na wasiwasi juu ya madhara hasi, lakini kwa wanawake wengi, hakuna shida. Kumbuka, unaingiza homoni mwilini mwako, kwahivyo inaweza kuchukua miezi michache mwili izoe. Ipe muda.Kuna vitu pengine vitaisha baada ya miezi 2 au 3:[2]
- kutokwa damu kati ya hedhi moja na inayofuata
- Ulaini wa matiti
- Kichefuchefu na kutapika
Vitu ambavyo vinaweza kuwa muda mrefu:
- Ongezeko la mchozo wa uke, mwasho au maambukizo
- Mabadiliko kwa tamaa yako ya ngono
Ikiwa baada ya miezi 3 unahisi kwamba madhara yamezidi kiwango unachoweza kuvumilia, tumia njia ingine uwe na kinga. Kumbuka, kuna njia kwa kila mtu, kila mahali!
* Kwa idadi ndogo mno ya wanawake, kuna hatari ya madhara makubwa.
Marejeleo
[1] Cook LA, et al. (2014). Vasectomy occlusion techniques for male sterilization (Review). John Wiley & Sons. Retrieved from https://www.cochranelibrary.com/cdsr/doi/10.1002/14651858.CD003991.pub4/full/es
[2] Dr Marie Marie Stopes International. (2017). Contraception. Retrieved from http://www.mariestopes.org.au/wp-content/uploads/Contraception-brochure-web-200417.pdf
[3] FPA the sexual health charity. (2015). Your guide to male and female sterilisation. Retrieved from https://www.fpa.org.uk/sites/default/files/male-and-female-sterilisation-your-guide.pdf
[4] FSRH Faculty of Sexual & Reproductive Healthcare. (2014). Male and Female Sterilisation. RCOG, London. Retrieved from https://www.fsrh.org/standards-and-guidance/documents/cec-ceu-guidance-sterilisation-cpd-sep-2014/
[5] Patil, E., & Jensen, J. T. (2015). Update on Permanent Contraception Options for Women. Current Opinion in Obstetrics and Gynecology. Retrieved from https://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC4678034/
[6] Reproductive Health Access Project. (2018). Permanent Birth Control (Sterilization). Retrieved from https://www.reproductiveaccess.org/wp-content/uploads/2014/12/sterilization.pdf
[7] RCOG Royal College of Obstetricians and Gynaecologists. (2016). Female Sterilisation. Royal College of Obstetricians and Gynaecologists, London. Retrieved from https://www.rcog.org.uk/globalassets/documents/guidelines/consent-advice/consent-advice-3-2016.pdf
[8] World Health Organization. (2016). Selected practice recommendations for contraceptive use. Geneva. Retrieved from https://apps.who.int/iris/bitstream/handle/10665/252267/9789241565400-eng.pdf?sequence=1
[9] World Health Organization Department of Reproductive Health and Research and Johns Hopkins Bloomberg School of Public Health Center for Communication Programs (2018) Family Planning: A Global Handbook for Providers. Baltimore and Geneva. Retrieved from https://apps.who.int/iris/bitstream/handle/10665/260156/9780999203705-eng.pdf?sequence=1