Mimba hutukia wakati mbegu kutoka mwilini mwa mwanamume inaporutubisha yai kutoka kwa mwili wa mwanamke. Mbegu inaweza kukutana na kurutubisha yai kwa njia nyingi tofauti:
- Shahawa hutoka ndani ya uume na kuinjia ndani ya uke
- Shahawa kuingia kwenye uke kupitia vidole
- Shahawa hutoka karibu na uke
- Kabla ya mbegu kuingia ndani au karibu na uke
- Shahawa kuingizwa katika uke kwa njia ya kuingizwa kibandia au yai lililorutubishwa nje ya mwili na kisha kuwekwa ndani ya tumboa la uzazi.
Hii ina maana kupenya si lazima kuwe na kupata mimba.