Kwa nini nitumie vidhibiti mimba?

Matumizi ya uzazi wa mpango hunufaisha kila mtu, jamii pana, na jamii kwa ujumla [1].Vidhibiti mimba vinakupa chaguzi; unaweza kuamua wakati ambapo unataka kupata watoto, unataka kuwa na watoto wangapi, na vilevile kama unataka kutopata watoto kabisa.
Vidhibiti mimba pia vinaleta hatari chache. Kwa mfano, vinaruhusu wanawake wachanga kungoja hadi wawe wakubwa na miili yao iweze kuhimili ujauzito; vile vile, wanaruhusu wanawake wazee kuzuia mimba wakati miili yao haiwezi tena kustahimili ujauzito na kuzaa.
Vidhibiti mimba huzuia mimba za utotoni, jambo ambalo linaweza kuathiri vibaya uhusiano na kazi zao. Mimba za utotoni pia zinaweza kuathiri vibaya afya ya mtoto mchanga kwani watoto wanaozaliwa na akina mama vijana huwa na uzito mdogo na ni hatari zaidi kwa sababu ya vifo vya watoto wachanga (mtoto anapokufa ndani ya siku 28).
Vidhibiti mimba huchangia watoto kuwa wenye afya bora kwa ujumla kwa sababu mimba zinapoachana kwa karibu sana husababisha kiwango cha juu cha vifo vya watoto wachanga (idadi ya vifo vya watoto wachanga chini ya umri wa mwaka mmoja). Hii ni kwa sababu wazazi wanaweza kutatizika wakitunza watoto wao wachanga wakati watoto wao wameachana kwa karibu sana.
Vidhibiti mimba huathiri vyema uchumi, mazingira, mfumo wa elimu na huduma za afya kwa sababu vinasaidia kupunguza kasi ya ongezeko la watu.