Mnong’onezaji wa mambo ya uke: Mambo yanayohatarisha uke na njia za kuitunza

Mnong’onezaji wa mambo ya uke: Mambo yanayohatarisha uke na njia za kuitunza

Uke ni sehemu moja ya mwili isiyoeleweka vizuri. Ingekuwa uke wako ungeweza kuongea,  ungekuambia nini? Nadhani unge changanyikiwa cha kusema. Mara tunaona makala inayosema safisha uke wako na tena baadaye tunaona ingine ikisema “kwanini kusafisha uke” ni hatari kufanya.
Kuna habari nyingi zisizo thibitishwa mtandaoni, mara nyingi, tunadanganywa kufanya hivi na vile ‘kutunza’ uke. Kwa ukweli, kutunza uke kunahusu tu kufanya maamuzi kubadilisha mtindo wa maisha ili uke uwe na afya bora.

Hatua ya kwanza ya utunzaji ni kubaini chanzo cha matatizo; Pata orodha hapa ya mambo yanayoweza kuhatarisha uke:

1) Wasiwasi

Haukutarajia hili liwe kwenye orodha, sivyo? Lakini wasiwasi unaweza kuleta hali ya ukosefu wa usawa kwenye homoni na hili linaweza kuleta matatizo kwenye  afya ya uke

Asian woman student or businesswoman work late at night. Concentrated and feel sleepy at the desk in dark room with laptop or notebook.Concept of people workhard and burnout syndrome. stress vagina health

Pia, kujikuna uke ni kawaida kwa wanawake wengine wanapokuwa na wasiwasi; Unawashwa na unajikuna na unahisi kujikuna zaidi kwasababu pengine una vijidonda vidogo vidogo vilivyosababishwa na kujikuna na vijindonda hivi huwasha na mzunguko wa kujikuna na kuwasha unaendelea.

2) Kemikali

Mara nyingi, tunaweka kemikali kwenye uke bila kujua. Tishu zilizo na marashi, sabuni za kusafisha uke, sabuni, sabuni za unga, dawa za kuuwa mbegu za kiume, mafuta za kulainisha, mafuta za uke na sabuni za kuosha zote huwa na kemikali. Ute ulio  kwenye ukuta wa uke hunyonya kemikali hizi haraka, kwahivyo ni bora upunguze kiwango cha kemikali kwa kukomesha  matumizi ya vitu kama  sabubi, sabubi za kusafisha uke, mafuta ya uke na pia utumie tishu zisizo na marashi.

Beautiful woman taking a bath and relaxing at home - lifestyle - feminine hygiene products

Tazama orodha ya viambato kwenye dawa ya kuuwa mbegu za kiume na mafuta za kulainisha kama zina kemikali za glycerin, petroleum jelly, nonoxynol 9, parabens na benzocaine ambazo hujulikana kuongeza ukuaji wa bakteria na mwasho wa ngozi (contact dermatitis)

3) chupi

Hili ni jambo la kushangaza, sindio? Aina ya chupi tunazovaa huathiri afya yetu ya uke zaidi kushinda tunavyofikiri.

Cropped studio shot of a group of beautiful young women posing together in their underwear vagina health

Ni vyema kutembea bila chupi lakini kwa wale hawawezi, hakikisha kuwa chupi sio za kubana kwani zinaweza kuzuia unyevu na ziwe eneo pa bakteria kukuwa au zisababishe nywele kutotoka nje ya ngozi (ingrown hair). Wakati unanunua chupi, tafuta inayokutosha vizuri haswa unaponunua G-string kwasababu G-string ndogo inaweza toa bakteria za mkundu izilete kwenye uke na kusababisha maambukizi kwenye njia ya mkojo.

4) Mlo

Vyakula huathiri uke na mwili kwa jumla. Uke yenye afya huwa na kiwango ya asidi ya asili (natural pH) na bakeria nyingi za afya bora; kuna vyakula hubadilisha kiwango cha asidi pH na kusababisha mabadiliko kwenye harufu ya uke.

Unhealthy snack at work time. Compulsive indulgence, overeating, stress, high calorie, fattening junk food, weight gain. Woman eating cookies at workplace vagina health

Pia, matatizo ya uke kama vile kuvimba (thrush) yanasemekana kuwa kawaida zaidi kwa watu walio na viwango vya juu vya glukosi na pia wakati mwingine ni dalili ya matatizo mengine kama mfumo wa kinga uliodhoofika.

5) Matendo ya ngono

Mangonjwa ya zinaa (STIs) ndio adui kubwa ya uke; kumbuka kila mara kutumia njia za uzuiaji mimba zinazozuia manii kama vile kondomu za ndani na nje ili kuepuka kupata STI na usisahau kutumia kondomu mpya ukiwa unabadilisha kutoka kwa mkundu kwenda kwenye uke.

Hand holding condom safe sex contraception STDs STIs

Kuwashwa kila mara, ute uliokuwa na rangi na harufu mbaya zinaweza kuwa dalili ya magonjwa ya zinaa (STIs).

6) Kulamba uke

Kulamba uke huleta raha, lakini ikipita kiasi kwa kuweka asali, krimu (kama ya keki), maziwa, juisi ya matunda, chokoleti au matunda kuifanya iwe tamu zaidi ni hatari na unaweza kupata uvimbe (thrush).

7) Kukauka na kujibana

Ebu fikiria hali mdomo wako hauna mate; hilo lina husu pia uke wako. Kuna aina nyingi ya majimaji ya ukeni na kutoka kwao ni jambo la kawaida; kuweka tamponi zako kwenye kemikali ya alkoholi ili kusitisha majimaji hizi kutoka ni jambo la hatari kwa uke.

Drop of cream from a tube - vagina tightening drying

Kubana uke pia ni tendo la hatari sana. Ukichunguza jinsi tembe na krimu za kubana uke hufanya kazi, utagundua kwamba kibana uke hukausha uke kwa muda mfupi na kuifanya ikae ndogo, hali inayoweza kusababisha machubuko na kukufanya uhisi uchungu wakati wa ngono.

Kuanzisha mabadiliko chanya

Jinsi bora zaidi ya kutunza uke wako ni kuijali kwa kukuwa mwenye huruma kwake kila mara.  Inamaanisha ufanye mabadiliko kwenye mtindo wa maisha. Unaweza fanya hivyo kwa njia hizi:

1) Masomo ya kuendelea

Unyanyapaa kuhusu  uke unaweza kupunguzwa tukisoma kuihusu na kufunza wengine.

2) Harakati chanya za uke

Kuna watu wanaotoa habari ya afya ya kijinsia kuhusiana na  uke; hili linasaidia watu wanaoishi maeneo ambayo yana rasimali chache kuhusu afya ya uke.

Fuata blogu na kurasa za mitandao ya jamii ambayo yanatoa habari zilizothibitishwa za kimatibabu  kuhusu uke.

3) Mazoea

Haitoshi kusoma kuhusu uke, kufanya kile ulichojifunza ndio hali ya juu ya kutunza uke. Ndio kwa sababu unastahili kupata habari zilizothibitishwa za kimatibabu  kuhusu uke.

Cha muhimu: Uke ni sehemu ya mwili inayoweza kustahimili mengi: Kuwa mwenye huruma kwake.

Je, una jambo la kusema?Wacha ujumbe wako hapa chini, wasiliana nasi kwenye kurasa zetu za mitandao ya  kijamii: Facebook, Instagram na Twitter au tutumie barua pepe kwenye info@findmymethod.org. Kwa taarifa zaidi kuhusu njia za uzuiaji mimba, tembelea  findmymethod.org

Kuhusu mwandishi: Amos Sanasi ni mdemografia, na mtaalamu wa maswala yanayohusiana na ngono na pia mwanzilishi wa jina la  rajamu la mambo chanya kuhusu ngono la kwanza nchini Nigeria, Revaginate NG ambalo linatoa taarifa za kina kuhusu ngono na vifaa vya ngono, haswa kwa watu walemavu. Yeye huandika kwenye akaunti ya twitter @thesanasi.